WOLVES WAMNG’ATA KOCHA WAO PEREIRA
Klabu ya Wolves inayoshiriki ligi kuu nchini Uingereza EPL imempiga kalamu meneja mkuu Vitor Pereira baada ya kushindwa kushinda mechi hata moja katika mechi 10 za ufunguzi wa msimu.
Pereira aliyetia Saini mkataba wa miaka 3 na kalbu hiyo mwezi Sptemba baada ya kuwaongoza Wanderers kuepuka kushushwa daraja msimu jana, aliandikisha pointi 2 pekee na Wolves katika mechi 10.
Msumari wa mwisho kwenye jeneza ulitiwa na kichapo cha mabao 3-0 mikononi mwa Fulham Jumamosi.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































