MAHAKAMA KUAMUA UUGIZAJI WA MCHELE
Mahakama ya Kerugoya kaunti ya Kirinyaga imeratibiwa kutoa uamuzi wake hii leo kuhusu iwapo serikali itaruhusiwa kuagiza mchele kutoka mataifa ya nje au la.
Hii ni baada ya chama cha wakulima wa mpunga kuwasilisha kesi mahakamani kupinga mpango wa serikali wa kuagiza tani elfu 500 za mchele ili kuziba pengo, waziri wa kilimo Mutahi Kagwe akisema wakulima nchini wamezalisha tani elfu 20 pekee.
Uamuzi huo utatolewa na jaji Edward Muriithi.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 







































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































