#Local News

ADA YA MATIBABU YA KARIUKI YAZIDI KUONGEZEKA

Familia ya mchuuzi aliyepigwa risasi ya mpira na kuwaachwa na majeraha mabayaitahitajika kulipia ada ya matibabu inayozidi shilingi milioni 2.

Jamaa zake Bonface Kariuki wanasema mwanao ambaye angalia anatumia mitambo ya kumweka hai hawezi kuzungumza wala kuwaona na hali yake haijabadilika ada ya matibabu nayo ikifikia shilingi milioni 2.3.

Haya yanajiri huku mkuu wa polisi kupitia kamanda wa polisi eneo la kati Samuel Ndanyi aliyetembelea familia yake akitoa hakikisho kuwa lazima Bonface atapata haki,polisi 2 waliomkabili wakiendelea kuzuiliwa.

Imetayrishwa na Maureen Mukhobe

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *