TANZANIA YAWATAKA RAIA KUSALIA NYUMBANI
Serikali ya Tanzania imewahimiza raia wake wasio watoaji wa huduma muhimu kusalia nyumbani wakati wa maadhimisho ya siku ya uhuru itakayoadhimisha hapo kesho nchini humo.
Katika taarifa ya msemaji wa serikali hiyo Mussa Azzan Zungu amewataka wafanyakazi wa huduma za dharura pekee kuripoti katika maeneo yao ya kazi.
Maadhimisho hayo yanajiri huku wito ukisheheni mitandaoni kuwataka wananchi kushiriki maandamano siku hiyo kulalamikia ukandamizaji wa haki za raia.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































