SEKTA YA AFYA YAENDELEA KUATHIRIKA
Masaibu yanayoikabili sekta ya afya yameendelea kuongezeka kutokana na migomo ya mara kwa mara, hii leo viongozi wa muungano wa madaktari KMPDU wakiwaongoza wanachama wake kuandamana jijini Nairobi kuikosoa serikali kutokana na kudorora kwa sekta hiyo.
Madaktari hao ambao wameungana na watumishi wengine wa umma, wameandamana kutoka hospitali ya kitaifa ya Kenyatta hadi katika makao makuu ya wizara ya afya, wakilalamikia masuala kadhaa ikiwemo kufeli kwa mfumo wa afya SHA.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































