#Local News

KeNHA YATAKIWA KUONDOA TRELA BARABARANI

Mamlaka ya barabara kuu nchini KeNHA imetakiwa kusaka barabara mbadala kwa malori ya masafa marefu yanayotumia barabara kuu ya Webuye kuelekea Kitale, ili kupunguza visa vya ajali ambavyo vimehusishwa na malori hayo.

Wakizungumza baada ya kuzitembelea familia za waathiriwa wa mkasa wa ajali katika eneo la Malaha Junction, mbunge wa Kimilili Didmus Barasa na mwenzake wa Narok West Gabriel Tongoyo, wamekariri kuwa barabara hiyo haina uwezo wa kuruhusu matumizi ya trela na magari ya uchukuzi wa umma.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *