KeNHA YATAKIWA KUONDOA TRELA BARABARANI
Mamlaka ya barabara kuu nchini KeNHA imetakiwa kusaka barabara mbadala kwa malori ya masafa marefu yanayotumia barabara kuu ya Webuye kuelekea Kitale, ili kupunguza visa vya ajali ambavyo vimehusishwa na malori hayo.
Wakizungumza baada ya kuzitembelea familia za waathiriwa wa mkasa wa ajali katika eneo la Malaha Junction, mbunge wa Kimilili Didmus Barasa na mwenzake wa Narok West Gabriel Tongoyo, wamekariri kuwa barabara hiyo haina uwezo wa kuruhusu matumizi ya trela na magari ya uchukuzi wa umma.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 



















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































