OCS TAALAM KUJUA HATMA KESHO
OCS wa kituo cha polisi cha Central Samson Taalam ataendelea kukesha katika kituo cha polisi cha Lang’ata hadi hapo kesho ambapo mahakama itaamua ombi lake la kupewa dhamana kwenye kesi inayomkabili kuhusiana na mauaji ya bloga Albert Ojwang.
Kwenye kesi hiyo, mamlaka ya kutathmini mienendo ya maafisa wa polisi IPOA imeomba mahakama itoe amri ya kumzuilia Taalam kwa siku 21 zaidi ili kukamilisha uchunguzi dhidi yake, ikizingatiwa kuwa amehusishwa moja kwa moja na mauaji hayo.
Imetayrishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































