RUTO ATAKUWA MGENI WA HESHIMA KATIKA SHEREHE ZA MIAKA 60 YA JESHI LA WANAHEWA

Rais William Ruto atakuwa mgeni wa heshima katika sherehe za kuadhimisha miaka 60 tangu kuanzishwa kwa Jeshi la Wanahewa la Kenya (KAF).
Hafla hiyo, itafanyika tarehe nane siku ya Jumamosi katika Kambi ya Ndege ya Moi mtaani Eastleigh kaunti ya Nairobi
KAF ni taasisi muhimu katika muundo wa Jeshi la Ulinzi la Kenya (KDF) na iliyotwikwa jukumu muhimu katika kulinda anga ya Kenya na uadilifu wa eneo
Imetayarishwa na Janice Marete