ODM YASHINIKIZA HAKI KWA WAATHIRIWA
Tukiwa bado katika masuala ya haki, chama cha ODM kimeitaka serikali kuharakisha fidia kwa familia zilizowapoteza wapendwa wao wakati wa maandamano nchini jinsi ilivyokubalika katika mkataba wa maelewano ya kisiasa baina ya chama hicho na UDA.
Wito huo ulitolewa kwenye hafla ya kumkumbuka aliyekuwa kinara wa ODM Raila Odinga, viongozi wakiitaka mahakama kuweka mbele haki kwa waathiriwa katika kesi ya kupinga kubuniwa kwa jopokazi la kushughulikia fidia hiyo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 












































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































