WAHADHIRI, SERIKALI WAKOSA MWAFAKA
Shughuli za masomo katika vyuo vikuu vya umma zimeendelea kuathirika kwa wiki ya 4 huku wahadhiri wakiitaka serikali iwape shilingi bilioni 9.7 za mishahara na marupurupu yao la sivyo waendelee na mgomo wao.
Wakiongozwa na katibu wa muungano wa UASU Dakta Constantine Wasonga, wahadhiri wamesema mgomo ungalipo licha ya serikali kutoa shilingi bilioni 4.3.
Hata hivyo, mazungumzo baina ya serikali na wahadhiri hao yamegonga mwamba, wahadhiri wakishinikiza kutekelezwa kikamilifu kwa makubaliano yao.
Wakati uo huo, Wasonga ameitaka serikali kuwaajiri wafanyakazi Zaidi wa vyuo vikuu.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 



















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































