#Local News

WAHADHIRI, SERIKALI WAKOSA MWAFAKA

Shughuli za masomo katika vyuo vikuu vya umma zimeendelea kuathirika kwa wiki ya 4 huku wahadhiri wakiitaka serikali iwape shilingi bilioni 9.7 za mishahara na marupurupu yao la sivyo waendelee na mgomo wao.

Wakiongozwa na katibu wa muungano wa UASU Dakta Constantine Wasonga, wahadhiri wamesema mgomo ungalipo licha ya serikali kutoa shilingi bilioni 4.3.

Hata hivyo, mazungumzo baina ya serikali na wahadhiri hao yamegonga mwamba, wahadhiri wakishinikiza kutekelezwa kikamilifu kwa makubaliano yao.

Wakati uo huo, Wasonga ameitaka serikali kuwaajiri wafanyakazi Zaidi wa vyuo vikuu.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

WAHADHIRI, SERIKALI WAKOSA MWAFAKA

MMOJA AUAWA KIMILILI, NYUMBA ZABOLEWA

WAHADHIRI, SERIKALI WAKOSA MWAFAKA

RUTO AAGIZA KUSITISHWA KWA USHIRIKIANO NA ADANI

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *