ANC YAPINGA TAARIFA ZA KUVUNJWA

Mwenyekiti wa chama cha ANC Kevin Lunami amepinga taarifa kwamba kuna mpango wa kukivunja chama hicho na kujiunga na UDA kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2027.
Lunami amesema ushirikiano uliopo baina ya chama hicho na serikali haimaanishi kuvunjwa kwa chama hicho, kauli yake ikiwiana na ya Katibu Mkuu wa chama hicho Omboko Milemba.
Hata hivyo, taarifa zinaashiria kuwa baraza kuu la ANC limeidhinisha kuvunjwa kwa chama hicho.
Imetayarishwa na: Antony Nyongesa.