HOMEBOYZ WAPOTEZA FURSA TENA
Klabu ya Kakamega Homeboyz ilipoteza fursa ya kurejea kileleni kwa ligi ya KPL, kufuatia sare ya goli 1 dhidi ya KCB FC hapo jana.
Homeboyz wana pointi 19 sawa na Gor Mahia, ila wanadunishwa na ubora wa mabao mbali na kucheza mechi 2 zaidi ya wenzao Gor.
Katika matokeo mengine, Shabana FC walikosa adabu na kutangaza ubabe wao, walipowalaza maafande wa Police FC kwa kichapo cha goli 1-0, nao Tusker FC wakirowesha sukari ya Mara Sugar kwa kichapo sawa.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 












































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































