MSAJILI WA WATU AAGIZWA KUFIKA MBELE YA MAHAKAMA YA ELDORET
Familia mbili zinakinzana kuhusu umiliki wa shamba la ekari 30 lenye thamani ya KSh. 30 milioni huko Uasin Gishu baada ya kuwasilisha vyeti vya kifo vinavyokinzana, vikimtaja marehemu Philip Cherono na Paul Kibet Cherono kama wamiliki wa awali.
Kutokana na mkanganyiko huo, Mahakama ya Eldoret imemwagiza Msajili Mkuu wa Watu kufika Julai 21 ili kutoa ufafanuzi kuhusu tofauti zilizopo kwenye majina na tarehe za vifo kabla ya kutoa uamuzi wa mwisho.
Imetayarishwa na Janice Marete
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































