KIPYEGON AVUNJA REKODI YAKE

Mkenya Faith Kipyegon alivunja rekodi yake ya dunia ya mbio za mita 1500 kwa wanawake katika mashindano ya Paris Diamond League hapo jana.
Hatua hiyo inakuja kama nyongeza ya wakati kwa bingwa wa Olimpiki mara mbili kabla ya Michezo ya Olimpiki ya Paris baadaye mwezi huu.
Jessica Hull wa Australia alitumia muda wa 3:50.83 na kumaliza wa pili, huku Laura Muir wa Uingereza akifunga akitumia muda wa 3:53.79 na kuchukua nafasi ya tatu.
Wakati huohuo, mshindi wa dunia wa medali ya fedha ya mita 800 Emmanuel Wanyonyi alifanya matokeo makubwa katika Ligi ya Diamond ya Paris, na kutwaa nafasi ya pili katika mchezo wa fainali dhidi ya Sedjati Djamel wa Algeria.
Mfaransa Gabriel Tual alishika nafasi ya tatu kwa muda wa 1:41.61, akimshinda Mkenya mwingine, Aaron Kemei, aliyemaliza wa nne kwa muda wa 1:42.08.
Bingwa wa Michezo ya Jumuiya ya Madola Wycliffe Kinyamal alifuatia kwa karibu katika nafasi ya tano, pia akitumia 1:42.08.
Imetayarishwa na Nelson Andati