UFISADI UNAANGAMIZA NCHI- MARAGA, KIGAME
Serikali imetakiwa kuvunja kimya chake kuhusu kudorora kwa sekta muhimu kama vile afya na elimu ya juu, ambayo imedorora kutokana na mgomo wa wahadhiri wa vyuo vikuu vya umma.
Wakizunguza katika hafla moja kaunti ya Makueni, jaji mkuu wa zamani David Maraga na mwimbaji wa nyimbo za injili Reuben Kigame, wamehusisha changamoto zinazoikabili nchi na ufisadi katika sekta mbali mbali.
Wawili hao waliotangaza azma ya kuwania urais, wamesema watatatua changamoto hizo iwapo watachaguliwa.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































