#Sports

OCHOLLA AFURAHISHWA NA KIKOSI CHAKE

Kocha Msaidizi wa KPA Samuel Ocholla amefurahishwa na juhudi na dhamira ya timu yake baada ya kupata ushindi wa mechi zote mbili wikendi katika Ligi Kuu ya Kikapu ya Wanawake nchini.
Siku ya Jumamosi, KPA iliishinda Strathmore Swords 73-51 na Jumapili wakaichapa ANU Panthers 83-39.
Ocholla alisisitiza kuwa timu hiyo itasalia na umakini kwani sasa ipo kileleni mwa msimamo wa ligi ikiwa na pointi 41 katika michezo 21, ikishinda 20 na kupoteza mmoja.

Imetayarishwa na Nelson Andati

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *