SERIKALI MBIONI KUIMARISHA UCHUMI WA BAHARI, MAZIWA
Rais William Ruto ameahidi kuwa serikali yake itaboresha miundomsingi katika sekta ya uchumi unaotegemea raslimali za baharini na maziwani ili kuboresha sekta hiyo na kuongeza mapato.
Rais ameyasema haya mjini Homa Bay kwenye kongamano la uchumi wa sekta hiyo, akisema serikali imewekeza shilingi bilioni 4 kwenye sekta hiyo.
Rais alikuwa ameandamana na kinara wa ODM Raila Odinga ambaye amehimiza usalama kuimarishwa kwenye Ziwa Victoria.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































