EACC YAPATA MKUU MPYA
Wakenya wanatarajia huduma zilizoimarika kutoka kwa tume ya maadili na kupambana na ufisadi EACC baada ya Abdi Ahmed Mohamoud kuapishwa rasmi kuwa afisa mkuu mtendaji wa tume hiyo kuhudumu kwa miaka 6 na kujaza nafasi ya Twalib Mbaraka aliyestaafu.
Mohamoud ameapishwa na jaji mkuu Martha Koome, akiahidi kuimarisha utendakazi wa tume hiyo na kupambana na walaji rushwa.
Aidha, amehimiza ushirikiano baina ya EACC na mahakama ili kukabili ufisadi.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































