#Local News

MWANGA WA TUMAINI NGARA

Wakazi wa eneo la Ngara Railway Southern Zone wamepata afueni baada ya mahakama kuu kutoa agizo la kuzuia mpango wa kufurushwa kutoka makazi yao.

Kwenye kesi hiyo, wakazi hao, wengi wao wakiwa wafanyakazi wa zamani wa shirika la Reli na wakongwe, wanahoji kuwa wameishi katika eneo hilo kwa miongo ambako wamewalea Watoto na wajukuu.

Kesi hiyo itasikilizwa tarehe 11 mwezi ujao.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *