SIWEZI TENA, GACHAGUA KUHUSU KUREJEA SERIKALINI
Aliyekuwa naibu rais Rigathi Gachagua amepuzilia mbali uwezekano wake kurejeshwa katika serikali ya rais William Ruto, anayosema ilimdhalilisha machoni pa wakenya.
Akizungumza kwenye mahojiano na vituo vya redio vinavyopeperusha matangazo kwa lugha ya Kiluhya, Gachaga amekariri kwamba hawezi tena kufanya kazi na serikali hiyo anayoitaja kuwa fisadi.
Wakati uo huo, Gachagua ameibua madai mapya kwamba Rais Ruto alitaka kumhongo kwa shilingi bilioni 2 ili ajiuzulu.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































