MASHIRIKA 47 YAVUNJWA
Kama njia mojawapo ya kubana matumizi ya fedha za umma baadaa ya kutupiliwa mbali mswada wa fedha wa mwaka 2024, Rais William ruto ametangaza mikakati ambayo imechukuliwa na serikali, ikiwemo kuvunja mashirika 47 ambayo huendesha shughuli zinazofanana.
Katika hotuba kwa taifa, Ruto amesema mashirika hayo hayajakuwa yakitengeneza faida, huku yakitumia mabilioni ya fedha za mlipa ushuru.
Aidha, Rais amesema majukumu ya mashirika husika na wafanyakazi wake watahamishiwa kwenye wizara mbali mbali.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































