IBADA YA MAZISHI YA ODINGA KUANZA
Ibada ya kitaifa ya mazishi ya waziri mkuu wa zamani Raila Odinga inatarajiwa kuanza muda wowote kuanzia sasa, ikiratibiwa kudumu kwa muda wa saa 2 pekee kuanzia saa tatu asubuhi katika uwanja wa michezo wa Nyayo.
Kwa mujibu wa mwenyekiti mwenza wa kamati ya kitaifa ya mazishi ya Odinga naibu Rais Kithure Kindiki, ibada hiyo pia itahudhuriwa na viongozi wa mataifa na serikali mbali mbali.
Mwili wa Odinga utapelekwa katika kaunti ya Kisumu hapo kesho kabla ya mazishi Jumapili.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































