#Local News

POLISI WALIOMJERUHI MCHUUZI KUSALIA NDANI KWA SIKU 15

Polisi 2 waliokamatwa baada ya kuonekana wakimpiga na kumjeruhi mchuuzi mmoja hapa Nairobi wakati wa maandamano watasalia ndani hadi tarehe 3 mwezi Julai.

Mahakama imeagiza wawili hao Barasa Masinde na Dancun Kiprono kuendelea kuzuiliwa kwa muda wa siku 15 ili kutoa nafasi ya kukamilishwa kwa uchunguzi dhidi yao.

Wawili hao walimjeruhi mchuuzi Bonface Mwangi Kariuki ambaye amelazwa katika hospitali ya Kenyatta katika chumba cha wagonjwa mahtuti.

Imetayrishwa na Maureen Mukhobe

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *