#Local News

RIPOTI YAFICHUA SHULE HEWA

Zaidi ya shule hewa 20 zimekuwa zikipokea mamilioni ya pesa katika kipindi cha miaka 4 iliyopita, mkaguzi wa hesabu za serikali Nancy Gathungu akiibua hofu kuhusu uwezekano wa wizara ya elimu kutumia mbinu hizo kufuja fedha za wakenya.

Kwenye ripoti ya uchunguzi ulioendeshwa katika shule 400 nchini, mkaguzi huyo aidha amebaini kuwa shule hizo hazimo katika sajili ya wakurugenzi wa elimu wa kaunti, licha ya uwepo wa akaunti za benki ambazo zimekuwa zikipokea fedha.

Aidha, amebaini kuwa shule zinakumbana na changamoto za kifedha, hatua ambayo huenda ikawalazimu wakuu wa shule kufunga shule mapema.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

RIPOTI YAFICHUA SHULE HEWA

HOFU YA UTEKAJI NYARA WEST POKOT

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *