WASAFIRI WATAKIWA KUJAZA FOMU YA HISTORIA YAO YA USAFIRI

Watu wanaoingia nchini sasa watatakiwa kujaza fomu kuhusu historia zao za usafiri kando na kufanyiwa vipimo vya ugonjwa wa mpox katika juhudi za kukabili maambukizi zaidi ya ugonjwa wa Mpox.
Katibu katika wizara ya afya Mary Muthoni amefichua kuwa wahudumu wa afya wametumwa katika mipanga mbal mbali ya nchi ili kuwafanyia vipimo wasafiri wanaokuja humu nchini huku akiwataka wakenya kukoma kueneza jumbe za uongo kuhusiana na ugonjwa wa Mpox.
Imetayarishwa na Janice Marete