#Local News

MATUMAINI YAPO KWA KENYA KUONGEZA MAPATO

Kenya bado inaweza kuongeza mapato zaidi kutokana na ushuru wa forodha na kusaidia ukuaji wa viwanda vyake vya ndani licha ya kuanguka kwa Mswada wa Fedha wa 2024.

Hii inafuatia uamuzi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kuipatia Kenya matakwa yake kuhusu mapendekezo kadhaa ya kutoza ushuru wa juu zaidi wa bidhaa zilizomalizika, huku ikiruhusu viwango vya chini vya malighafi kusaidia uzalishaji wa ndani.

Inajumuisha simu za rununu, seti za runinga kati ya vifaa vingine vya elektroniki, vifaa vya kuchezea, mafuta ya kula, na diapers, kati ya zingine.

Hii ni chini ya Ushuru wa Pamoja wa Nje wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (CET) ambayo ina bendi nne zenye kiwango cha chini cha asilimia 0, viwango vya asilimia 10, asilimia 25 na kiwango cha juu cha asilimia 35, kwa bidhaa zote zinazoagizwa kutoka kwa mataifa mengine.

Sehemu ya nne ya asilimia 35 ilipitishwa Mei 2022 ili kusaidia kulinda na kudumisha uwekezaji uliopo katika kanda na kuhimiza viwanda vya ndani, uongezaji wa thamani na uanzishaji wa viwanda.

Hata hivyo nchi zimekuwa zikitafuta viwango vya juu au vya chini kwa bidhaa maalum ili kujaribu kusawazisha mahitaji husika.

Imetayarishwa na Janice Marete

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *