#Local News

MSHUKIWA WA UGAIDI GRANT AFUKUZWA KENYA BAADA YA KUMALIZA KIFUNGO CHA JELA

Mshukiwa wa ugaidi wa Uingereza jana Alhamisi alirejeshwa nyumbani kwao Uingereza, kutoka Kenya Jermaine Grant alifungwa jela kwa kumiliki vifaa vya kutengeneza bomu na kughushi.

Alihusishwa na Mjane Mzungu Samantha Lewthwaite ambaye hayupo.

Polisi na maafisa wa uhamiaji wanasema kufukuzwa kwake kumetokea baada ya kumaliza kifungo chake gerezani.

Grant amerudishwa Uingereza akiandamana na maafisa wa Kenya na kukamatwa mara moja baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Heathrow.

Mahakama ya Mombasa mwaka jana ilikuwa imeamuru Grant afurushwe nchini mara baada ya kifungo chake gerezani kukamilika kufuatia kesi iliyowasilishwa na waendesha mashtaka kutaka afurushwe.

Maafisa wa usalama wanaamini Grant ana uhusiano na Mjane Mweupe, mke wa mshambuliaji wa kigaidi wa 7/7 Germaine Lindsay, na al-Shabaab.

Imetayarishwa na Janice Marete

MSHUKIWA WA UGAIDI GRANT AFUKUZWA KENYA BAADA YA KUMALIZA KIFUNGO CHA JELA

OMBI LA KUBATILISHA UTEUZI WA BARAZA JIPYA

MSHUKIWA WA UGAIDI GRANT AFUKUZWA KENYA BAADA YA KUMALIZA KIFUNGO CHA JELA

ANSELMINO AINGIA CHELSEA

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *