KESI DHIDI YA GAKUYA KUREJELEWA
Kesi ya ufisadi inayohusu madai ya ufujaji wa shilingi milioni 40 inayomkabili mbunge wa Embakasi North James Gakuya inarejelewa hii leo katika mahakama inayosikiliza kesi zinazohusiana na ufisadi jijini Nairobi.
Gakuya aanakabiliwa na mashtaka manne ikiwemo mgongano wa maslahi kwa madai kwamba alitoa kandarasi za ujenzi wa barabara kwa kampuni zilizo na uhusiano wa karibu naye.
Mashtaka mengine ni njama ya ulaghai, ukiukaji wa sheeria za ununuzi na uporaji wa mali ya umma.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































