WATANO WAFARIKI KWENYE MGODI RONGO

Watu 5 wamefariki baada ya ukuta wa mgodi kuporomoka na kuwaangukia walipokuwa wakichimba migodi katika eneo la Rongo kaunti ya Migori.
Akithibitisha kisa hicho, Naibu Kamishna wa kaunti ndogo ya Rongo George Matundura, amesema watu zaidi wangali wamekwama kweny mgodi huo na kuongeza kwamba juhudi za uokozi zinaendelea.
Aidha, ameahidi kwamba serikali itaweka mikakati ya kuimarisha usalama wa shughuli za uchimbaji migodi eneo hilo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa