MPOX YARIPOTIWA TENA NCHINI

Kisa cha tatu cha virusi vya nyani yaani Mpox kimeripotiwa nchini, huku mkurugenzi mkuu wa afya Dakta Patrick Amoth akisema mwathiriwa ni wa kike mwenye umri wa miaka 30 aliyekuwa amerejea jijini Nairobi baada ya safari nchini Uganda. Kulingana na Amoth, mwathiriwa alirejea nchini baada ya safari ya wiki jana, na anapokea matibabu akiwa katika […]

WALIMU WAANDAMANA NAIROBI, WAAPA MGOMO UNGALIPO

Walimu wa shule za sekondari wamelemaza masomo kwa siku ya 5 mfululizo kote nchini wakiitaka tume ya kuwaajiri walimu TSC itekeleze mkataba wa maelewano wa kati ya mwaka 2021-25 ikiwemo kuwapa makataba wa kudumu walimu wa JSS. Jijini Nairobi, walimu hao wameandamana hadi katika afisi za TSC wakisisitiza kwamba mgomo utaendelea hadi mkataba wao utekelezwe. […]

WANAFUNZI TURKANA WAANDAMANA KUPINGA UHAMISHO WA MWALIMU

Wanafunzi wa shule ya mseto ya upili ya Kalobeyei eneo la Kakuma kaunti ya Turkana wameandamana na kutembea kwa umbali wa kilomita 30 hadi katika afisi ya mkurugenzi wa elimu eneo hilo wakilalamikia hatua ya tume ya TSC kumhamisha mwalimu mkuu wa shule hiyo. Kwa mujibu wa wanafunzi hao, mwalimu aliyehamishwa amekuwa akichangia matokeo bora […]

MNYAMA ASIYEFAHAMIKA ALETA JOTO LIKUYANI

Wakazi wa Kijiji cha Lugulu eneo bunge la Likuyani kaunti ya Kakamega wanaishi kwa hofu kutokana na madai kwamba wamemwona mnyama asiyefahamika ikivamia mifugo wao. Wakizungumza na wanahabari, wakazi hao wamesema kwamba hofu hiyo imeathiri masomo huku wakihofia usalama wa wanao wanapoelekea shuleni. Aidha, wameitaka idara ya wanyamapori nchini KWS kuingilia kati na kumnasa mnyama […]

WALIMU WA CHEKECHEA WALALAMIKIA AJIRA MIEZI MBILI BAADA YA KUPEWA KANDARASI YA KUDUMU

Walimu wa shule za chekechea katika kaunti ya Pokot Magharibu wameibua lalama miezi miwili tu baada ya gavana wa kaunti hiyo Simon Kachapin kuwapa kandarasi ya kudumu. Kwa mujibu wa katibu mkuu wa muungano wa walimu wa chekechea katika kaunti hiyo Joseph Sarich kndarasi walizopewa walimu hao haziendani na kanuni zilizowekwa na tume ya kuratibu […]

WAKENYA WAHIMIZWA KUKUMBATIA MAISHA CARD

Wakenya wanahimizwa kubadilisha vitambulisho vyao na kuchukua vya kisasa maarufu Maisha card kwa kujwa Serikali inapanga kutumika vipengee bora zaidi katika card hiyo kwa manufaa ya mwananchi. Katibu katika wizara ya uamiaji Julius Bitok anasema kuwa ingawaje wakenya bado watakubaliwa kutumia vitambulisho vyao vya kisasa katika uchaguzi mkuu ujao vipengee vya juu vya kidijitali katika […]

WALIMU WA CHEKECHEA WALALAMIKIA AJIRA MIEZI MBILI BAADA YA KUPEWA KANDARASI YA KUDUMU

Walimu wa shule za chekechea katika kaunti ya Pokot Magharibu wameibua lalama miezi miwili tu baada ya gavana wa kaunti hiyo Simon Kachapin kuwapa kandarasi ya kudumu. Kwa mujibu wa katibu mkuu wa muungano wa walimu wa chekechea katika kaunti hiyo Joseph Sarich kndarasi walizopewa walimu hao haziendani na kanuni zilizowekwa na tume ya kuratibu […]

RAIS RUTO AZINDUA MRADI WA NISHATI YA SOLA MAGETA

Wakaazi wa kaunti ya siaya eneo la kisiwa cha mageta wanatarajiwa kunufaika na mradi wa nishati ya sola ambao umezinduliwa na rais William Ruto katika eneo hilo. Akihutubu wakati wa uzinduzi wa mradi huo ambao utagharimu kima cha shilingi milioni 230 rais Ruto amefichua kuwa mradi huo unalengo la kuhakikisha kwamba wakaazi wa eneo hilo […]

WAHUDUMU WA TUK TUK KAKAMEGA WAFUNGA NJIA

Makabiliano makali yameshuhudiwa katika mji wa Kakamega maafisa wa polisi wakikumbwa na wakati mgumu kuwakabili waendeshaji wa TukTuk waliokuwa wamefunga barabara za kuingia mjini humo wakilalamikia hatua ya afisa wa polisi aliyempiga risasi mteja akiwa ndani ya tuk tuk jana alhamisi akimwaangaisha dereva hujyo kwa kuitisha hongo. Kwa mujikbu wa wahudum u hao afisa huyo […]

WAKAAZI WA TRANSNZOIA WANUFAIKA NA MRADI WA MAJI

Ni afueni kwa wakaazi wa kaunti ya Transnzoia baada ya Gavana wa kaunti hiyo George Natembea kuwahakiishia kuwa kampuni ya kusambaza maji itaboreshwa hata zaidi ili kusambaza maji kwa wakaazi wote. Kulingana na natembeaya wakati wa wateja wa maji kulimbikiziwa bili za maji umepita na kwamba kila mmoja atalipa kulingana na matumizi yake. Imetayarishwa na Janice Marete