MACHOGU APUUZA KAULI ZA WALIMU WAKUU

Waziri wa elimu Ezekiel Machogu, ameendelea kupuzilia mbali kauli za baadhi ya walimu wakuu wa shule za umma kwamba watafunga shule mapema kutokana na mgao wa elimu.
Akizungumza jijini Nairobi, Machogu amesema mgao huo utatolewa kwa wakati ufaao.
Hata hivyo, mwenyekiti wa chama cha wazazi Cyrus Obuhatsa, amesema sughuli za masomo katika shule za umma zinatatizika kutokana na kucheleweshwa kwa mgao huo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa