IPOA YACHUNGUZA KIFO KITUO CHA POLISI
Mamlaka huru ya kuchunguza mienendo ya polisi IPOA imeanzisha uchunguzi kufuatia kifo cha mshukiwa aliyeripotiwa kujitoa uhai katika kituo cha polisi cha Kisumu central.
Kulingana na taarifa ya polisi, mwili wa mwendazake aliyetambuliwa kama Kelvin Oduor ulipatikana ukiwa unaning’inia kwenye dirisha la bafu la kituo hicho cha polisi.
Marehemu alikuwa amekamatwa kwa madai ya wizi na vurugu na kushtakiwa kabla ya mahakama kuamrisha azuiliwe kwa siku 14 kukamilisha uchunguzi.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 









































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































