WAZIRI WA ELIMU MACHOGU AAGIZA HELB KUFUNGUA TOVUTI YA UFADHILI KWA WANAFUNZI KUTUMA MAOMBI
Waziri wa Elimu Ezekiel Machogu ameamuru Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HELB) na Hazina ya Vyuo Vikuu (UF) kufungua tovuti ya ufadhili kuanzia Juni 15, ili kuruhusu wanafunzi wanaohitimu kutuma maombi yao
Amri hiyo inajiri baada ya Rais William Ruto mwezi Mei kutambulisha muundo mpya wa ufadhili kwa wanafunzi wa vyuo vikuu na na vyuo vya kiufundi TVET nchini Kenya, kufuatia mashauriano ya kitaifa yaliyofanywa na Chama cha Rais kuhusu Marekebisho ya Elimu.
Imetayarishwa na Janice Marete
English 



















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































