MAFUTA YAPUNGUA KWA SHILINGI 1
Bei ya mafuta ya petroli imepungua kwa shilingi moja kila lita huku ile ya diseli na mafuta taa ikisalia jinsi ilivyokuwa kwa kipindi cha mwezi mmoja uliopita.
Hii baada ya mamlaka ya kudhibiti kawi EPRA kutoa bei mpya za bidhaa hiyo kwa kipindi cha kati ya tarehe 15 mwezi huu hadi tarehe 14 mwezi ujao, ikisema bei ya uagizaji wa mafuta kutoka nje ilipungua kwa kiasi kidogo.
Lita ya petroli jijini Nairobi sasa itauzwa kwa shilingi 185.31, nayo diseli na mafuta taa ikisalia shilingi 171.58 na 155.58 mtawalia.
Imetayarishwa na Maureen Amwai
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































