KHRC YAIBUA WASI WASI KUHUSU WAADHIRIWA WA MAFURIKO

Tume ya kutetea Haki za Kibinadamu ya Kenya (KHRC) imeibua wasi wasi kuhusu mpango wa kuhamishwa kwa familia zilizoathiriwa na mkasa wa Mai Mahiu Huku ikitoa wito wa kuwepo kwa uwazi,
Tume hiyo imeshutumu serikali kwa kufurusha familia kutoka kambi mbili hadi kwenye nyumba za kukodi bila kutoa suluhu la kudumu kwa muda mrefu.
Haya yanajiri huku serikali ikifunga kambi mbili za mwisho zilizokuwa zikihifadhi familia hizo na kuwapa fidia kodi ya nyumba ya miezi mitatu licha ya baadhi ya waathiriwa kukataa hatua hiyo
Imetayarishwa na Janice Marete