WAZAZI WAWATAKA WALIMU KURUDI SHULENI

Muungano wa kitaifa wa wazazi umewataka walimu kufutilia mbali mgomo wao ambao umeratibiwa kuanza wiki ijayo shule zitakapofunguliwa kwa muhula wa tatu.
Mwenyekiti wa kitaifa wa muungano huo Silas Obuhatsa, amehofia kudhoofika kwa masomo wakati huu ambapo wanafunzi wanafaa kujiandaa kwa mitihani ya kitaifa.
Aidha, ameitaka miungano ya walimu KNUT na KUPPET kuangazia upya uamuzi wao.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa