MAHAKAMA YAAGIZA KUSITISHA UJENZI WA KANISA KATIKA IKULU
Mahakama Kuu imetoa agizo la kusitisha kwa muda ujenzi wa majengo yoyote ya kudumu ya kidini, yakiwemo makanisa, katika Ikulu hapa Nairobi, na makazi mengine rasmi ya serikali kote nchini.
Agizo hilo lilitolewa na Jaji Chacha Mwita kufuatia ombi kutoka kwa shirika la Transparency International Kenya, Tume ya kutetea Haki za Kibinadamu ya Kenya, na makundi mengine mawili.
Jaji Mwita, anasema kuwa masuala yaliyoibuliwa ni mazito na yanahitaji mahakama kuingilia kwa haraka ili kuruhusu uchunguzi zaidi wa kisheria.
Imetayarishwa na Maureen Mukhobe
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































