WATU WANNE WAFARIKI KATIKA AJALI BARABARA YA MARSABIT-MOYALE
Watu wanne wamefariki na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya basi walilokuwa wakisafiria kuhusika katika ajali ya barabarani eneo la Gof Chopa barabara ya Marsabit-Moyale.
Basi hilo lilikuwa likitoka Nairobi kuelekea Moyale kupitia Marsabit ajali hiyo ilipotokea.
Majeruhi wanapokea matibabu katika hospitali ya rufaa ya kaunti ya Marsabit huku miili ya marehemu ikihifathiwa katika chumba cha maiti cha kituo hicho.
Imetayarishwa na Janice Marete
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































