#Local News

PETER WANYAMA AKUBALI MATOKEO LSK

Wakili Peter Wanyama amekubali matokeo ya uchaguzi wa chama cha wanasheria nchini LSK wa hapo jana ambapo alimaliza wa pili nyuma ya mshindi Charles Kanjama, ila akalalamikia alichokitaja kuwa kutojitolea kwa mawakili kushiriki uchaguzi huo.

Wanyama ambaye alitangaza kuwania kiti hicho Septemba mwaka jana, amesisitiza kuwa uongozi unahiaji unyenyekevu katika kushinda na kushindwa.

Amesema licha ya mawakili wanaohudumu kuwa 18,000 kati ya 26,000 walio wanachama wa LSK, ni 8,600 pekee waliojitokeza kupiga kura.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *