UASU WATISHIA KUGOMA

Muungano wa wafanyikazi wa vyuo vikuu umetoa notisi ya siku saba ya mgomo kulalamikia kucheleweshwa na kutolipwa mishahara yao yote.
Katibu mkuu wa UASU Constantin Wesonga ametangaza kuwa notisi hiyo itaanza kutumika mara moja na kutishia kulemaza masomo katika vyuo vikuu vyote vya umma wakati ambapo wanafunzi wapya na wanaoendelea watakaporipoti shuleni.
Imetayarishwa na Janice Marete