WATU 4 WAFARIKI WAKICHIMBA MIGODI YA DHAHABU MOYALE MARSABIT
Watu wanne wamethibitishwa kuaga dunia katika maeneo ya uchimbaji madini ya Hillo kaunti ndogo ya Moyale kaunti ya Marsabit huku mamlaka ikijitahidi kuzima shughuli hiyo haramu ya uchimbaji madini.
Naibu Kamishna wa Kaunti ya Moyale Benedict Munyoki amesema kuwa wachimba migodi ambao baadhi yao hawana kibali cha kuchimba migodi walifanikiwa kujipenyeza katika eneo la operesheni na kuanza kuchimba madini hayo na kusababisha vifo vya watu wanne baada ya migodi hiyo kuzama.
Imetayarishwa na Janice Marete
English 







































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































