#Football #Sports

KAHATA AWEKA MATUMAINI KWA KCB

Kiungo mshambuliaji wa zamani wa Gor Mahia, Francis Kahata, ameonyesha matumaini kuwa bao lake la kwanza litakuwa mwanzo wa mafanikio mema kwa klabu yake mpya huku nusu ya pili ya ligi ikianza.

Kiungo huyo mkongwe alipachika bao wakati KCB iliposhinda Posta katika ushindi muhimu uliopatikana kwenye Uwanja wa Kasarani

Bao hilo lilikuwa la kwanza la ligi kwa kahata huku akisema mafanikio hayo ni mwanzo wa mwelekeo mpya wanapolenga kupanda juu kwenye msimamo wa ligi na kupata matokeo zaidi.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *