#Local News

UPASUAJI WA MIILI YA MAFURIKO KUFANYWA 

Zoezi la upasuaji wa miili ya watu waliofariki kutokana na mafuriko wiki jana jijini Nairobi imeratibiwa hii leo katika makafani ya City, baada ya miili hiyo kutambuliwa huku idadi ya waliofariki kote nchini ikifikia watu 44.

Familia za walioangamia zimekuwa zikifika katika makafani hayo tangu Jumamosi kwa lengo la kuwasaka na kuwatambua jamaa zao waliosombwa na maji ya mafuriko Ijumaa usiku.

Serikali ya kaunti ya Nairobi imefutilia mbali bili zote za hospitali kwa waathiriwa wa mafuriko hayo.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *