MVUA KUBWA KUENDELEA KUNYESHA NCHINI, UTABIRI WAONYESHA

Idara ya utabiri wa hali ya anga imesema mvua kubwa inatarajiwa kuendelea kunyesha katika kaunti za magharibi, Nairobi, Bonde la ufa na ziwa Victoria wikendi hii.
Kwenye taarifa, idara hiyo imeonya kuwa Alhamisi ijayo, mvua kubwa itanyesha jijini Nairobi na kutatiza shughuli za usafiri, na kuwataka wakazi kuchukua tahadhari.
Utabiri huo unatofautiana na ule uliotollewa Jumatano wiki hii kwamba hapatakuwa na mafuriko tena, ila mvua kubwa.
Imetayarishwa na: Antony Nyongesa
English 



















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































