#Local News

HUDUMA KENYA YATAKIWA KUPIGA JEKI MIRADI YA SERIKALI

Idara ya huduma Kenya imetakiwa kupiga jeki juhudi za serikali kuhakikisha kuwa wakenya Zaidi wanajisajili kwenye bima ya Taifa Care.

Akizungumza kwenye kongamano la mameneja vituo vya Huduma Center jijini Mombasa, katibu katika wizara ya utumishi wa umma Amos Gathecha ameitaka idara hiyo pia kuorodhesha idadi ya wakenya waliosajiliwa kupitia huduma Kenya.

Aidha, ametoa hakikisho kuwa changamoto za vifaa vya kidijitali zitaondolewa hivi karibuni kwenye idara hiyo.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *