#uncategorized

POLISI WANASA PIKIPIKI 59 ZILIZOIBWA

Polisi mjini Eldoret wamewakamata watu wanne akiwemo mmiliki wa karakana baada ya kuwanasa na pikipiki 59 na sehemu 35 za injini zilizokuwa zimeibwa kutoka kwa wahudumu wa bodaboda katika kaunti ya Uasin Gishu.

Akiwahutubia wanahabari katika kituo cha polisi cha Central mjini humo, kamanda wa polisi Benjamin Mwathi amesema pikipiki hizo zimenaswa katika karakana eneo la Kapsoya baada ya kudokezewa na wananchi.

Aidha, amesema washukiwa wanatarajiwa kufikishwa mahakamani.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

POLISI WANASA PIKIPIKI 59 ZILIZOIBWA

TUWE NA SUBIRA ASEMA BARRY

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *