ODINGA ASHUTUMU ‘AMRI YA KUUA’ YA MURKOMEN
Kinara wa ODM Raila Odinga amemshutumu waziri wa usalama Kipchumba Murkomen kutokana na amri ya Murkomen ya kuwataka polisi wawapige risasi watakaokaribia kituo cha polisi, Odinga akiitaja amri hiyo kuwa ya kiholela.
Akizungumza kwenye hafla moja katika eneo la Bondo, Odinga amemtaka Murkomen kuiheshimu sheria, inayowataka polisi kuwalinda raia Pamoja na mali zao.
Hata hivyo, Murkomen amejitetea akisema alinukuliwa visivyo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 












































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































