POLISI WAWILI WAKAMATWA KIRINYAGA

Maafisa wawili wamekamatwa kwa madai ya kushirikiana na mshukiwa wa mauaji raia wa Uganda katika kaunti ya Kirinyaga.
Mshukiwa huyo anayedaiwa kutoroka katika kituo cha polisi cha Kiamasiri alikamatwa mwezi uliopita kwa tuhuma za mauaji ya mwajiri wake novemba mwaka jana.
Kwa mujibu wa familia ya marehemu mshukiwa alitoroka ijumaa wiki iliyopita kabla ya kufikishwa mahakamani leo hii.
Imetayarishwa na Janice Marete.