#Sports

DORTUMUND YAFUZU KWA 16 BORA

Bao pekee la kipindi cha kwanza lililofungwa na Daniel Svensson liliipa Borussia Dortmund ushindi wa 1-0 dhidi ya Ulsan HD Jumatano huku Wajerumani hao wakifanikiwa kutinga hatua ya 16 bora ya Kombe la Dunia la Vilabu.

Ushindi wa pili mfululizo wa Dortmund kwa tofauti ya bao moja, kufuatia kichapo cha 4-3 dhidi ya Mamelodi Sundowns siku ya Jumamosi, ulitazamwa na watazamaji zaidi ya 8,000 pekee mjini Cincinnati, miongoni mwao Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance na mkuu wa FIFA Gianni Infantino.

Inamaanisha kuwa Dortmund wanafuzu kwa hatua ya 16 bora kama washindi wa Kundi F, huku Fluminense wakipita nyuma yao katika nafasi ya pili baada ya kuizima Sundowns katika sare ya bila kufungana iliyochezwa wakati huo huo huko Miami.

Imetayrishwa na Nelson Andati

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *