WANAFUNZI SITA WAFARIKI KWENYE AJALI YA BARABARA YA KITUI – KIBWEZI
Watoto sita wa shule wamefariki katika ajali ya barabarani katika kituo cha biashara cha Wiitu kwenye barabara ya Kitui-Kibwezi.
Akithibitisha kisa hicho cha Naibu Kamishna wa Ikitha Vincent Loctary Lomachary, amesema walioathiriwa ni pamoja na watoto watatu wa shule ya msingi na watatu wa shule ya upili.
Kulingana na naibu kamishna wa kaunti, wanafunzi hao waliangushwa na gari aina ya Probox walipokuwa wakivuka barabara.
Imetayarishwa na Janice Marete
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































